Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Masikini Wema! Atupwa mahabusu
Habari MchanganyikoMichezo

Masikini Wema! Atupwa mahabusu

Wema Sepetu (mwenye gauni jeusi) akitolewa mahakamani na kupelekwa mahabusu
Spread the love

WEMA Sepetu, mwigizaji na msanii maarufu wa filamu nchini, amejisalimisha na kutupwa mahabusu baada ya Mahakama ya Kisutu, jijini Dar es Salaam kuagiza kusakwa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Maira Kasonde, Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo tarehe 11 Juni 2019, alitoa amri ya kumkamata Wema popote alipo baada ya kushindwa kufika mahakamani ili kusikiliza kesi yake inayohusu kuchapisha video chafu mtandaoni.

Msanii huyo amekamatwa leo tarehe 17 Juni 2019, katika Mahakama ya Kisutu baada ya mahakama hiyo kutoa wito wa kukamatwa kwake.

Alipofika mahakamani, Wema alikamatwa na kupandishwa kwenye gari la Magereza na kupelekwa Segerea. Anatarajiwa kufikishwa mahakamani hapo tarehe 24 Juni 2019. Siku hiyo mahakama itaamua kumfutia dhamana ama la!

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

error: Content is protected !!