Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Sheikh wa Dodoma ahimiza amani nchini
Habari Mchanganyiko

Sheikh wa Dodoma ahimiza amani nchini

Sheikh wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mustapha Rajabu
Spread the love

SHEIKH wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mustapha Rajabu amewataka Watanzania kuishi maisha ya kulinda na kutunza  amani. Anaripoti Danson Kaijage … (endelea).

Ameyasema  hayo wakati akitoa ujumbe wa Sikukuu ya Eid katika msikiti wa Gaddafi jijini Dodoma, kuwa amani iliyokuwa imetawala kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani inatakiwa kuendelezwa kila siku.

Aidha amesema, Watanzania wanatakiwa kumuogopa Mwenyezi Mungu kwa kuacha kufanya mambo mabaya ikiwemo wizi, mauaji, kupora na kufanya yale mazuri yanayoleta maendeleo katika ngazi ya familia hadi ngazi ya Taifa.

“Wakati tunafanya mashindano ya Quran  pale uwanja wa Jamhuri tulimuomba kamanda wa polisi (Gilles Muruto) ulinzi tukihofia kutokea matukio ya kihalifu, lakini chakufurahisha lile gari la polisi lilikuwa sehemu moja mpaka tukamaliza mashindano hayo, hiyo ni ishara ya kuwa kila mtu anajua umuhimu wa kufanya yale yanayompendeza Mwenyezi Mungu,” amema Sheikh Rajabu.

Pia aliongeza kuwa Waislamu wanatakiwa kuishi maisha ya kusaidiana kama ilivyokuwa kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani, huku akisema wapo ambao baada ya mwezi mtukufu wa Ramadhani kuisha watarudia kufanya yale waliyokuwa wakiyafanya kipindi cha nyuma.

Awali akizungumza, sheikh alisema maisha ambayo watanzania watanakiwa kuishi maisha ya kutobaguana kwa sababu ya dini au kabila, akisema katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani  hata wale ambao sio Waislamu walishiriki kwenye matukio mbalimbali mfano kufuturisha, ikiwa ni ishara ya kuonyesha Watanzania ni kitu kimoja.

Akizungumza mmoja ya waamini wa dini ya kiislamu, ambae pia ni mkazi wa Dodoma alisema watayaenzi yale waliyokuwa wanayafanya katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa kuwasaidia watoto yatima pamoja na watu wengine wenye uhitaji maalumu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Balile aukwaa uenyekiti wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

Habari Mchanganyiko

Jeshi la Uhifadhi kujengewa uwezo zaidi

Spread the love  WIZARA ya Maliasili na Utalii imejipanga vyema kuendelea kulijengea...

Habari Mchanganyiko

Wanavyuo Dodoma waonja utamu wa chimbo la nyuki

Spread the love  TAMASHA la Chimbo la Nyuki lililofanyika katika Ukumbi wa...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

error: Content is protected !!