Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Lukuvi aagiza taasisi wadaiwa pango la ardhi kukutana naye
Habari Mchanganyiko

Lukuvi aagiza taasisi wadaiwa pango la ardhi kukutana naye

Spread the love

WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, imeagiza taasisi za umma na watu binafsi zaidi 200 zinazodaiwa kodi ya pango la ardhi na malimbikizo ya muda mrefu, kuhudhuria kikao maalum kitachofanyika tarehe 11 Juni 2019, jijini Dodoma. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea). 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa tarehe 5 Juni 2019 na Dorothy Mwanyika, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, taasisi hizo zitakaposhindwa kufika katika kikao hicho, hatua za kufuta milki zao na kuuza viwanja husika zitafuata kwa mujibu wa sheria.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa, mashirika, taasisi na makampuni yanayodaiwa kodi ya pango la ardhi yanatakiwa kufika na nyaraka za umiliki pamoja na stakabadhi za malipo yote yaliyofanyika,  katika kikao hicho baina yao na Waziri wa Wizara hiyo, William Lukuvi.

Aidha, taarifa hiyo imetoa wito kwa wadaiwa hao kwenda kulipia madeni yao kwa hiari, katika ofisi za ardhi zilizoko karibu na maeneo yao, kwa kuwa ofisi hizo ziko wazi siku zote.

Miongoni mwa taasisi hizo ni pamoja na Exim Bank Tanzania Limited, Efatha Ministry, Dar es Maritime Institute, CRDB Bank PLC, College Business Education, Chuo cha Ushirika Moshi (MUCCOB), Bodi ya Korosho Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!