Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo TP Mazembe kutua kesho, kuivaa Simba
Michezo

TP Mazembe kutua kesho, kuivaa Simba

Haji Manara
Spread the love

KLABU ya soka kutoka nchini DR Congo TP Mazembe inatarajia kuwasili nchini kesho kwa ajili ya mchezo wa Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Simba utakaochezwa Jumamosi ya tarehe 6, Aprili katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es Salaam. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Afisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa wapinzani wao wanatarajia kutua kesho majira ya saa saba mchana, tayari kwa mchezo wao wa raundi ya kwanza wa robo fainali ambapo kiingilio cha chini cha mchezo huo kitakuwa Sh. 4,000.

“Tumeweka viingilio rafiki sana kwa mashabiki wetu ili waweze kuja kushabikia timu yao uwanjani, ambapo kiingilio cha chini kitakuwa Sh. 4,000 na mpaka sasa tiketi zimeshaanza kuuzwa kwa mawakala wote,” Haji Manara

Msemaji huyo aliongezea kuwa tiketi za mchezo wao dhidi ya TP Mazembe za bei ya chini zitauzwa mwisho Ijumaa ambapo ikifika siku ya Jumamosi zitauzwa kwa Sh. 5,000 ili kuepusha msongamano siku ya mechi.

Simba imefanikiwa kufuzu robo fainali kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kushika nafasi ya pili kwenye D baada ya kufanikiwa kupata ushindi kwenye mchezo wa mwisho dhidi ya AS Vita.

Mara ya mwisho timu hizo zilikutana mwaka 2011 katika hatua ya mtoano, ambapo mchezo wa kwanza uliochezwa Lubumbashi, Simba ilifungwa mabao 3-1, katika mchezo wa marudiano uliochezwa April 4, 2011 kwenye Uwanja wa Taifa, TP Mazembe iliibuka tena na ushindi wa mabao 3-2.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

error: Content is protected !!