Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Chadema ahoji uharaka wa serikali kubinafsisha viwanda
Habari za Siasa

Mbunge Chadema ahoji uharaka wa serikali kubinafsisha viwanda

Devotha Minja, Mbunge wa Viti Maalum Chadema
Spread the love

MBUNGE wa Viti Maalum, Devotha Minja (Chadema) amehoji serikali sababu za kushindwa kufanya maandalizi mazuri katika ubinafsishaji wa viwanda? Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Na kwamba, badala yake viwanda vingi kwa sasa vimebaki kuwa sehemu za kuishi popo, mbunzi na ng’ombe.

Akiuliza swali la nyongeza bungeni leo tarehe 2 Aprili 2019 amesema, lengo la serikali kubinafsisha viwanda ilikuwa kuboesha uzalishaji.

Na kwamba, kwa sasa kinyume chake, hivyo amehoji, ni kwanini serikali ilikuwa na uharaka wa kubinafsisha wa viwanda hivyo?

“Lengo la serikali kubinafsisha viwanda ilikuwa ni kuongeza ufasisi, kuendelea kuwepo kwa viwanda visivyofanya kazi, serikali haioni kwamba imeshindwa kutimiza wajibu wake”

“Hivi kulikuwa na uharaka gani wa serekali kubinafsisha viwanda hivyo bila kuwaandaa wawekezaji,” amehoji Minja.

Awali katika swali la msingi la mbunge huyo, alitaka kujua ni lini serikali itatekeleza ahadi  iliyotolewa wakati wa kampeini 2015 za kutaka kuwapatia vijana ajira?

Mhandisi Stella Manyanya, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara akijibu maswali hayo amesema kuwa, mpango wa serikali ni kuhakikisha viwanda vyote vilivyobinafsishwa na visivyofanya kazi vinafufuliwa ili vichangie katika uchumi na kutoa ajira kwa vijana.

Amesema, pia serikali inahamasisha ujenzi wa viwanda vipya kwa kutegemeana na fursa zinazopa nchini.

“Mkoa wa Morogoro una viwanda 14 vilivyobinafsishwa, kati ya viwanda hivyo ni viwanda nane vinavyofanya kazi na viwanda sita havifanyi kazi.

“Wizara yangu kwa kushirikiana na ofisi ya msajili wa hazina, tumefanya tathimini ya viwanda vilivyobinafsishwa nchini vikiwemo viwanda vya Mkoa wa Morogoro,” alisema Mhandisi Manyanya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!