Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif apigwa ‘stop’ Clouds TV
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif apigwa ‘stop’ Clouds TV

Spread the love

MAMLAKA katika kituo cha televisheni cha Clouds, jijini Dar es Salaam, imeagiza kufutwa kwa mahojiano kati ya kituo hicho na mwanasiasa mkongwe Visiwani Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mahojiano kati ya Maalim Seif na kituo hicho, yalipangwa kufanyika leo, tarehe 28 Machi na kurushwa moja kwa moja (live), kupitia kipindi kilichopewa jina la Clouds 360.

Kwa mujibu wa Ado Shaibu, katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama cha ACT-Wazalendo, televisheni ya Clouds ndiyo iliyoomba kuwapo mahojiano hayo na Maalim Seif.

Anasema, “Clouds TV imefuta ratiba ya mahojiano hayo kwa kile walichoeleza, sababu zilizo nje ya uwezo wao.”

Maalim Seif ambaye amewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) na Makamu wa Kwanza wa Rais katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Alijiunga na ACT- Wazalendo na kukabidhiwa kadi ya heshima ya mwanachama Na. 1, mapema wiki iliyopita, kufuatia Mahakama Kuu, kumtangaza Prof. Ibrahim Lipumba, kuwa mwenyekiti halali wa chama hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

error: Content is protected !!