Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Mahenge: Kupandisha bei hakutawasaidia
Habari Mchanganyiko

Dk. Mahenge: Kupandisha bei hakutawasaidia

Spread the love

MKUU wa mkoa wa Dodoma, Dk. Binilith Mahenge amewataka wafanyabiashara wa Dodoma kufanya biashara zao kwa malengo ya kujiongezea kipato kwa njia harari badala ya kupandisha bei ya bidhaa wanazouza. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kwa Niaba ya Mkuu wa Mkoa, Diwani wa kata ya Matumbulu, Emmanuel Chibago alisema kuwa mkuu wa mkoa amemtuma ili kuweza kuwashauri wafanyabiashara hao waweze kutambua yakuwa uuzaji wa bidhaa ni sehemu ya kutoa huduma na siyo kuwakomoa walaji kwa kuwapandishia bei.

Diwani huyo alikutanana wafanyabiashara wa soko kuu la majengo kwenye mkutano wao mkuu wa kikatiba uliofanyika jijini Dodoma.

Akizungumza kwenye mkutano huo aliwataka wafanyabishara hao kufanya biashara zao kwa malengo ya kujiletea kipato kitakachowawezesha kujipatia mikopo, badala ya kuelekeza kwenye mtizamo ya kupandisha bei mazao yao.

Alisema pamoja na wafanyabiashara kuwa na changamoto mbalimbali zinazowakabili bado Serikali kwa kupitia halmashauri ya Jiji tayari imeanza kutoa fedha  kwa ajili ya ukarabati kwenye baadhi ya maeneo ambayo miundombinu imeharibika na kupoteza hadhi ya kusababisha soko hilo.

“Serikali inatambua changamoto zilizopo kwenu  wafanyabishara wa masoko yaliyopo ndani ya jiji hili, lakini hata hivyo tayari hatua zimeanza kuchukuliwa ikiwa na pamoja na ukarabati ulioanza kwenye soko kuu hili la Majengo kwa upanuaji wa paa ambayo yalikuwa yakivuja,” amesema Chibago.

Awali akisoma risala kwa mkuu huyo wa mkoa wa Dodoma, Mwenyekiti wa soko kuu la Majengo, Hamisi Bomu alisema kuwa pamoja na malengo waliyokuwanayo ya kutaka kujiinua kiuchumi kwa kupitia biashara bado wana changamoto zinazowafanya kutofikia hatua mzuri.

Alitaja changamoto hizo ni pamoja na kuvuja  kwa paa la soko, uwepo wa mkataba usio shirikishi kwa upande mmoja, miundombinu mibovu, eneo lililotengwa la stockyard kutokuwa na kivuli, vifaa vya usafi vichache ikiwa na pamoja na uwepo wa biashara holela pembezoni mwa soko.

Alisema soko hilo limekuwa likihudumia zaidi ya watu 8000 na kuwezesha halmashauri kukusanya mamilioni  ya fedha kwa mwezi yanayotokana na ushuru, lakini bado ahadi za utatuzi na marekebisho ya kasoro hizo umekuwa mgumu.

Hata hivyo pamoja na changamoto iliyopo uongozi wa soko utaendelea kuwaunganisha wafanyabishara kuwa wamoja katika kutafuta maslahi yao na maendeleo na kutafuta sauti moja ya mawasiliano kati yetu na halmashauri ya jiji na taasisi za kiserikali na kiraia kwa ajili ya kufikia malengo ya kukuza mitaji inayotokana na vyanzo vya mapato yetu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari Mchanganyiko

Shahidi aeleza namna Nathwani alivyomjeruhi jirani yake

Spread the loveMSIMAMIZI wa Msikiti wa Wahindi Lohana aitwae, Ankit Dawda (32)...

error: Content is protected !!