Tuesday , 30 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba ‘out’ Sport Pesa
Michezo

Simba ‘out’ Sport Pesa

Wachezaji wa Bandari FC wakishangilia ushindi wao dhidi ya Simba na kutinga hatua ya fainali ya michuano ya Sport Pesa
Spread the love

SIMBA imeondoshwa katika michuano Sport Pesa baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Bandari FC ya Kenya katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… (endelea)

Simba walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa mshambuliaji wao Meddy Kagere dakika ya 45, Bandari FC wakafanikiwa kusawazisha bao hilo kwa njia ya mkwaju wa penalti katika dakika ya 59 kupitia kwa William Wadri

Katika kipindi cha pili Simba walifanya mabadiliko na kuingiza wachezaji watano wakiwemo Emanuel Okwi, Pascal Wawa, Jonas Mkude, Shiza Kichuya na Haruna Niyonzima lakini ilipofika dakika ya 72 mchezaji Wilberforce Lugogo alifanikiwa kuipatia Bandari FC bao la pili ambalo lilidumu mpaka mwisho na kufanikiwa kuingia fainali.

Ikumbukwe bingwa wa michuano hiyo atapata zawadi ya kombe na kiasi cha fedha Sh. 30 milioni sambamba na kucheza mechi na klabu ya Evarton FC inayoshiliki Ligi Kuu nchini England mwezi Julai mwaka huu.

Tazama mabao yote hapo chini

https://www.youtube.com/watch?v=IRIX5pQq48Y

 

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

error: Content is protected !!