Wednesday , 27 September 2023
Home Kitengo Michezo Simba ‘out’ Sport Pesa
Michezo

Simba ‘out’ Sport Pesa

Wachezaji wa Bandari FC wakishangilia ushindi wao dhidi ya Simba na kutinga hatua ya fainali ya michuano ya Sport Pesa
Spread the love

SIMBA imeondoshwa katika michuano Sport Pesa baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Bandari FC ya Kenya katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… (endelea)

Simba walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa mshambuliaji wao Meddy Kagere dakika ya 45, Bandari FC wakafanikiwa kusawazisha bao hilo kwa njia ya mkwaju wa penalti katika dakika ya 59 kupitia kwa William Wadri

Katika kipindi cha pili Simba walifanya mabadiliko na kuingiza wachezaji watano wakiwemo Emanuel Okwi, Pascal Wawa, Jonas Mkude, Shiza Kichuya na Haruna Niyonzima lakini ilipofika dakika ya 72 mchezaji Wilberforce Lugogo alifanikiwa kuipatia Bandari FC bao la pili ambalo lilidumu mpaka mwisho na kufanikiwa kuingia fainali.

Ikumbukwe bingwa wa michuano hiyo atapata zawadi ya kombe na kiasi cha fedha Sh. 30 milioni sambamba na kucheza mechi na klabu ya Evarton FC inayoshiliki Ligi Kuu nchini England mwezi Julai mwaka huu.

Tazama mabao yote hapo chini

https://www.youtube.com/watch?v=IRIX5pQq48Y

 

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

BiasharaMichezo

Piga pesa kupitia Derby ya London Kaskazini kwa kubadhiri na Meridianbet

Spread the love NAJUA umesikia na unazijua Derby nyingi kutoka jiji la London,...

error: Content is protected !!