Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wavuvi 16 wa Tanzania kuburuzwa mahakamani Kenya
Habari za Siasa

Wavuvi 16 wa Tanzania kuburuzwa mahakamani Kenya

Spread the love

WAVUVI takribani 16 kutoka Tanzania wamekamatwa nchini Kenya Jumapili tarehe 18 Novemba 2018, kwa madai ya kuingia nchini humo kinyume na sheria na kutumia vifaa haram vya uvuvi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Watanzania hao wanadaiwa kukamatwa katika ufukwe wa Bamgot karibu na Ziwa Victoria ulioko Kaunti ya Migori, na kupelekwa kwenye kituo cha polisi cha Macalder huku boti zao zikizuiliwa na Jeshi la Polisi.

Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Migori, Joseph Nthenge amesema watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi juu ya madai yao kukamilika, ambapo kwa sasa maafisa wa polisi wanawahoji.

Sekeseke la wavuvi katika nchi zinazozunguka na kutumia ziwa Victoria, limepamba moto baada ya siku za hivi karibuni, wavuvi wa Kenya wanaotumia ziwa hilo, kudaiwa kukamatwa na vyombo vya dola vya nchi za Tanzania na Uganda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!