Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Waitara: Wathubutu waone
Habari za SiasaTangulizi

Waitara: Wathubutu waone

Spread the love

NAIBU Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mwita Waitara amesisitiza kuwa, marufuku ya wazazi kuchangishwa michango ya wananfunzi shuleni ibaki pale pale na kwamba, walimu wasithubutu kukiuka agizo hilo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Waitara ambaye ni Mbunge wa Ukonga, Dar es Salaam kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) ametamka hayo wakati wa ziara ya kushukuru wananchi wa jimbo lake waliopo kwenye Kata ya Chanika ikiwa ni baada ya kumalizika kwa vikao vya Bunge Ijumaa iliyopita.

Akiwa kwenye ziara hiyo jimboni kwake Waitara amesema, utaratibu wa kuwaandikisha watoto wote waliofika uamri wa kwenda shule katika elimu ya awali na msingi unapaswa kutekelezwa kwa kuwa ndio sheria inavyoelekeza.

Mbunge huyo ambaye awali alitokana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amewaeleza wakati wa Chanika kuwa, ataendelea na oparesheni ya kuhakikisha wanafunzi wanaandikishwa shule huku akiahidi kuwa, wataothubutu kukwamisha utekelezwaji wa agizo hilo kutokana na michango atakiona.

“Nasimamia kwa karibu suala la elimu, michango yenye kero imeondolewa, watoto darasa la awali, la kwanza na kidato cha kwanza waandikishwe, hii ni oparesheni ya kuhakikisha wanaandikishwa.

“Ni marufuku kuzuia mwanafunzi kujiunga darasa la awali, la kwanza na kidato cha kwanza kama mzazi wake hajatoa michango, ukizuiliwa kuandikisha mtoto sababu hujatoa mchango toa taarifa,” amesema Waitara.

Amesema Serikali inakataza michango yenye kero hivyo atakayezuia watoto kuandikishwa kwa sababu hiyo atachukuliwa hatua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!