Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tamaa ya cheo imempeleka Mtolea CCM
Habari za Siasa

Tamaa ya cheo imempeleka Mtolea CCM

Spread the love

HAMAHAMA ya wabunge, madiwani na wanasiasa wa upinzani ndani ya vyama vyao na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) imeelezwa kuwa inasababishwa uroho wa nyadhifa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano, Abdallah Kambaya amesema kuwa wabunge na madiwani wamekimbia vyama vya upinzani na kujiunga na chama tawala ili watafute fursa za watawala.

Kuhama kwa Mbunge wa Temeke ambaye alijinasibu kuwa yeye sio manafki na hatohama upinzani.

Amesema kuwa Mtolea hana sababu za msingi za Kujiunga na CCM isipokuwa ni tamaa ya nyadhfa kama ile aliyokuwa nayo Mtatiro.

Mtulia huyu huyu ndiye aliyekuwa mstari wa mbele kuisema serikali ya CCM kuhusu shambulio la Lissu bungeni leo ameungana na wale aliwawalalamikia.

“Mtulia alikwenda Liwale akatumia jukwaa la kampeni kumtukana Kuchauka leo hii ameenda alipoenda kuugana naye”.amesema Kambaya.

“Tabia hii ya kuhama na kusaliti imekuwa ikiendelezwa na wabunge wa CUF wanaomunga mkono Maalimu Seif Sharif Hamad ambao wamekuwa wakijinasabu kuwa wao ndio imara sisi tunatumika” amesema.

Wakati huo huo amemtaja Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa CUF Julias Mtatiro kuwa amehama upinzani kwa tamaa ta kupata nyadhifa kama kama walivyoapa kina Katambi.

“Hii tabia ya kina Mtatiro ni Tabia ya Ujokate na Tabia ya Umakonda,” amesema Kambaya.

Kambaya amemtaja Mbunge wa Kinondoni Maulidi Mtulia kuwa alihama CUF kutokana na kutumia vibaya ubunge wake,
amedai kuwa mbunge huyu alikopa fedha nyingi alizoshindwa kuzilipa na hivyo aliamua kuhama ili anze upya na apate tena stahiki za ubunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!