Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tamaa ya cheo imempeleka Mtolea CCM
Habari za Siasa

Tamaa ya cheo imempeleka Mtolea CCM

Spread the love

HAMAHAMA ya wabunge, madiwani na wanasiasa wa upinzani ndani ya vyama vyao na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) imeelezwa kuwa inasababishwa uroho wa nyadhifa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano, Abdallah Kambaya amesema kuwa wabunge na madiwani wamekimbia vyama vya upinzani na kujiunga na chama tawala ili watafute fursa za watawala.

Kuhama kwa Mbunge wa Temeke ambaye alijinasibu kuwa yeye sio manafki na hatohama upinzani.

Amesema kuwa Mtolea hana sababu za msingi za Kujiunga na CCM isipokuwa ni tamaa ya nyadhfa kama ile aliyokuwa nayo Mtatiro.

Mtulia huyu huyu ndiye aliyekuwa mstari wa mbele kuisema serikali ya CCM kuhusu shambulio la Lissu bungeni leo ameungana na wale aliwawalalamikia.

“Mtulia alikwenda Liwale akatumia jukwaa la kampeni kumtukana Kuchauka leo hii ameenda alipoenda kuugana naye”.amesema Kambaya.

“Tabia hii ya kuhama na kusaliti imekuwa ikiendelezwa na wabunge wa CUF wanaomunga mkono Maalimu Seif Sharif Hamad ambao wamekuwa wakijinasabu kuwa wao ndio imara sisi tunatumika” amesema.

Wakati huo huo amemtaja Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa CUF Julias Mtatiro kuwa amehama upinzani kwa tamaa ta kupata nyadhifa kama kama walivyoapa kina Katambi.

“Hii tabia ya kina Mtatiro ni Tabia ya Ujokate na Tabia ya Umakonda,” amesema Kambaya.

Kambaya amemtaja Mbunge wa Kinondoni Maulidi Mtulia kuwa alihama CUF kutokana na kutumia vibaya ubunge wake,
amedai kuwa mbunge huyu alikopa fedha nyingi alizoshindwa kuzilipa na hivyo aliamua kuhama ili anze upya na apate tena stahiki za ubunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!