Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Takukuru yamhoji Sethi
Habari Mchanganyiko

Takukuru yamhoji Sethi

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo tarehe 8 Novemba 2018 imeelezwa kwamba mtuhumiwa katika kesi ya uhujumu uchumi, Harbinder Sethi amechukuliwa maelezo yake na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wakili wa Takukuru, Leornad Swai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ameieleza mahakama hiyo kuwa, jana walifanikiwa kuchukua maelezo ya Sethi.

Wakili Swai ameieleza mahakama kuwa, baada ya Takukuru kuchukua maelezo ya Sethi, wanaendelea na hatua za upelelezi zinazofuata.

Kufuatia kauli hiyo, Wakili wa Sethi, David Chillo aliutaka upande wa mashtaka kuharakisha upelelezi wa kesi hiyo.

Hakimu Shaidi kutokana na maelezo ya pande zote mbili, aliiahirisha kesi hiyo hadi tarehe 22 Novemba 2018, siku ambayo tarehe itakapotajwa, pamoja na kuangalia kama upelelezi umekamilika au bado.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Shahidi aeleza namna Nathwani alivyomjeruhi jirani yake

Spread the loveMSIMAMIZI wa Msikiti wa Wahindi Lohana aitwae, Ankit Dawda (32)...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

error: Content is protected !!