Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Takukuru yamhoji Sethi
Habari Mchanganyiko

Takukuru yamhoji Sethi

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo tarehe 8 Novemba 2018 imeelezwa kwamba mtuhumiwa katika kesi ya uhujumu uchumi, Harbinder Sethi amechukuliwa maelezo yake na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wakili wa Takukuru, Leornad Swai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ameieleza mahakama hiyo kuwa, jana walifanikiwa kuchukua maelezo ya Sethi.

Wakili Swai ameieleza mahakama kuwa, baada ya Takukuru kuchukua maelezo ya Sethi, wanaendelea na hatua za upelelezi zinazofuata.

Kufuatia kauli hiyo, Wakili wa Sethi, David Chillo aliutaka upande wa mashtaka kuharakisha upelelezi wa kesi hiyo.

Hakimu Shaidi kutokana na maelezo ya pande zote mbili, aliiahirisha kesi hiyo hadi tarehe 22 Novemba 2018, siku ambayo tarehe itakapotajwa, pamoja na kuangalia kama upelelezi umekamilika au bado.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!