Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Takukuru yamhoji Sethi
Habari Mchanganyiko

Takukuru yamhoji Sethi

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo tarehe 8 Novemba 2018 imeelezwa kwamba mtuhumiwa katika kesi ya uhujumu uchumi, Harbinder Sethi amechukuliwa maelezo yake na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wakili wa Takukuru, Leornad Swai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ameieleza mahakama hiyo kuwa, jana walifanikiwa kuchukua maelezo ya Sethi.

Wakili Swai ameieleza mahakama kuwa, baada ya Takukuru kuchukua maelezo ya Sethi, wanaendelea na hatua za upelelezi zinazofuata.

Kufuatia kauli hiyo, Wakili wa Sethi, David Chillo aliutaka upande wa mashtaka kuharakisha upelelezi wa kesi hiyo.

Hakimu Shaidi kutokana na maelezo ya pande zote mbili, aliiahirisha kesi hiyo hadi tarehe 22 Novemba 2018, siku ambayo tarehe itakapotajwa, pamoja na kuangalia kama upelelezi umekamilika au bado.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!