MAMLAKA ya Udhibiti wa Nishati, Maji na Mafuta (EWURA) imetangaza ongezeko la bei za mafuta ya petroli, diseli na mafuta ya taa, yaliyoshushwa katika bandari ya Dar er Salaam na Tanga. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Akitangaza bei za mafuta kwa mwezi Novemba mwaka huu jana jijini Dar es Salaam, Meneja Mawasiliano EWURA, Titus Kaguo alisema diseli iliyoshushwa katika bandari ya Dar es Salaam imepanga kwa Sh. 81 kwa lita wakati petroli iliyoshuhswa kwenye bandari hiyo ikipanda kwa Sh. 29.
Kaguo alieleza kuwa, diseli iliyoshushwa kwenye bandari ya Tanga imepanda kwa Sh. 111 kwa lita na petroli iliyoshushwa katika bandari hiyo imepanda kwa Sh. 87 kwa lita.
Kufuatia mabadiliko hayo, Kaguo alisema mafuta ya Petroli kwenye mkoa wa Dar es Salaam yatauzwa Sh. 2,396 kwa lita na diseli itauzwa Sh. 2,385.
Aidha, alisema bei ya mafuta yaliyoshushwa katika bandari ya Mtwara imebaki pale pale, kutokana kwamba hakuna mafuta yaliyoingizwa bandarini hapo mwezi uliopita.
Kaguo alisema sababu za bei ya mafuta kupanda ni kupanda kwa bei za mafuta katika soko la dunia pamoja na gharama za ucheleweshaji bandarini.
Leave a comment