Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TCU watia kitanzi vyuo viwili
Habari Mchanganyiko

TCU watia kitanzi vyuo viwili

TCU
Spread the love

TUME ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) imevifuta vyuo vikuu viwili kikiwemo cha Mtakatifu Yohana (SJUT) kilichopo Msalato Dodoma na Theophil Kisanji (TEKU) cha Tabora na kusitisha utoaji mafunzo katika vyuo vikuu vitano. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Wakati akizungumza na wanahabari leo tarehe 25 Septemba 2018 jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa amevitaka vyuo vilivyositishwa kutoa mafunzo kuwahamisha wanafunzi katika vyuo vilivyositishwa kuhamishwa katika vyuo vingine kabla ya muhula wa mwaka wa masomo wa 2018/19 kuanza.

Profesa Kihampa, amevitaja vyuo vilivyositishwa kutoa mafunzo ikiwemo Chuo Kikuu cha Bagamoyo (UoB), Chuo Kikuu cha Eckernford Tanga (ETU), Chuo Kikuu cha Mlima Meru, Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta kituo cha Arusha (JKUAT-Arusha Center) na Chuo Kikuu Kishiriki cha Josiah Kibira (JOKUCo).

Amesema vyuo hivyo viko katika uangalizi maalum na kwamba haviruhusiwi kudahili wanafunzi wapya kwa ngazi zote za masomo kuanzia Astashahada, Stashahada, Shahada, Shahada ya uzamili na uzamivu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

error: Content is protected !!