Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Mafia inasubiri ya MV Nyerere?
Makala & UchambuziTangulizi

Mafia inasubiri ya MV Nyerere?

Spread the love

NAWAKUMBUSHA tu wale mahodari wa kutuma salaam za rambirambi, na wakukataza majanga ya ajali yasigeuzwe mtaji wa kisiasa,  wakumbuke na Kisiwa cha Mafia kabla ya janga jingine kutokea. Anaandika Babu Jongo…(endelea).

Kwa miaka zaidi ya 50 tangu tupate uhuru, bado wakazi wa kisiwa cha Mafia kilichopo mkoani Pwani wanatumia usafiri huu wa boti za mbao, zisizokuwa na usalama wowote kutoka na kuingia kisiwani humo.

Boti hizi zenye kuhatarisha maisha ya wananchi wa Mafia na wageni wengine, ndio kiunganishi kikubwa kati ya kisiwa cha Mafia na maeneo mengine kama Dar es Salaam na hata wilaya nyingine za mkoa wa Pwani.

Kila siku boti hizi husafiri umbali wa km 30, kutoka Kisiwani Mafia mpaka Nyamisati wilayani Kibiti, huku zikiwa na uwezo wa kubeba wastani wa watu 45 – 70.

Wabunge wote waliopata kuongoza jimbo la Mafia walihaha kupata kivuko cha uhakika bila mafanikio.

Hata mbunge wa sasa ameshafanya juhudi kubwa kuiomba serikali kuitazama Mafia kwa jicho la huruma bila mafanikio.

Ameshawahi kuiomba serikali ya chama chake impe hata lile boti lililokuwa linachukua saa tatu kusafisha abiria kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo, lakini akaambulia matupu.

Naikumbusha tu serikali, kwamba rambirambi zao wasichange mapema wanunue boti ya uhakika kusafirisha wananchi wa Mafia, ambao kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012, kisiwa hicho kilikuwa na wakazi wapatao 52,000.

Naamini kwa jitihada za mheshimiwa rais kutoa elimu bila malipo, watu watakuwa wameongezeka sana hasa baada ya rais kusema wazaane tu kwa kuwa elimu ni bure.

Toeni rambirambi mapema mnunue kivuko kuwavusha wakazi wa Mafia, msisubiri kuchanga rambirambi baada ya kufa kwa uzembe!

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Maafa Manyara: Rais Samia akatisha ziara yake Dubai

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amekatisha ziara yake...

Habari za SiasaTangulizi

Wataalaam wa miamba watua Hanang

Spread the loveWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na...

Habari za SiasaTangulizi

ACT Wazalendo washtushwa vifo 47 mafuriko Hanang

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeelezza kupokea kwa mshtuko na simanzi...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!