Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Michezo TFF wawatia kitanzi waamuzi wanne
Michezo

TFF wawatia kitanzi waamuzi wanne

Spread the love

SHIRIKISHO la mpira wa miguu Tanzania TFF, kupitia kamati yake ya uendeshaji wa ligi (Kamati ya Masaa 72) iliyokaa jumamosi imewatia hatiani waamuzi wanne wanao chezesha ligi kuu kwa kushindwa kutafsili sheria 17 za mchezo wa soka katika baadhi ya mechi walizocheza. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Waamuzi waliokutwa na rungu hilo ni Jimmy Fanuel, Jamada Ahmada, Athumani Lazi na Nicholas Makaranga.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura amesema kamati hiyo ilikaa na kupitia mikanda ya video ya baadhi ya michezo iliyokuwa na maamuzi yenye upungufu kutoka kwa waamuzi.

“Kamati ilipitia taarifa za michezo mbali mbali na kuangalia matukio yaliyojitokeza na ilifanya maamuzi kulingana na kanuni mbalimbali za mashindano za ligi husika,” amesema Wambura.

Hata hivyo katika hatua nyingine kamati hiyo ya Saa 72, imevipiga faini ya Sh. 500,000, klabu za Coastal Union, Mbao FC na Prisons kila mmoja kwa kushindwa kuwadhibiti washabiki wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

error: Content is protected !!