Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makontena ya Makonda kupigwa mnada J’mosi
Habari za Siasa

Makontena ya Makonda kupigwa mnada J’mosi

Spread the love

BAADA ya mnada wa kwanza wa makontena 20 yenye samani yaliyoingizwa na Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kukwama, Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imepanga kufanya mnada wa pili Jumamosi ya Septemba mosi, 2018. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

TRA imetaarifu kuwa, imedhamiri kurudia mnada huo wa makontena yenye samani za ofisi ikiwemo meza na viti, ambayo yamekwama katika bandari kavu ya Dar es Salaam kutokana na kudaiwa kodi ya kaisi cha Sh. 1.2 bilioni.

Mamlaka hiyo imetoa wito kwa wananchi kujitokeza katika mnada huo kununua samani hizo kwa kufuata taratibu na sheria za minada.

Aidha, TRA imewatoa hofu wananchi kuhusu kauli iliyotolewa na Makonda ya kwamba atakaye nunua makontena hayo atalaaniwa na Mungu.

Baada ya mnada wa kwanza uliofanyika tarehe 25 Agosti, 2018 kukwama kutokana na wateja kushindwa kufika bei elekezi, Makonda alitoa kauli akisema kuwa, mtu atakayenunua makontena hayo atapata laana kwa kuwa, makontena hayo yenye samani yaliingizwa nchini kwa ajili ya kuwasaidia waalimu wa mkoa wa Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!