Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dada wa Rais Magufuli afariki dunia
Habari za SiasaTangulizi

Dada wa Rais Magufuli afariki dunia

Spread the love

MONICA Joseph Magufuli, Dada wa Rais John Magufuli amefariki dunia asubuhi ya leo tarehe 19 Agosti, 2018 kwenye Hospitali ya Bugando iliyoko jijini Mwanza alikokuwa anafanyiwa matibabu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa za kifo hicho zimetolewa na Gerson Msigwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu kupitia ukurasa wake wa Instergram.

“Nasikitika kuwajulisha kuwa Dada wa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bi. Monica Joseph Magufuli amefariki dunia asubuhi leo tarehe 19 Agosti, 2018 katika hospitali ya Bugando Jijini Mwanza alikokuwa akipatiwa matibabu. Natoa pole kwa Rais Dk. John Joseph Magufuli, Familia ya Mzee Joseph Magufuli, Ndugu, Jamaa na wote walioguswa na msiba huu. Raha ya milele umpe e Bwana na mwanga wa milele umuangazie, Marehemu Monica Jospeh Magufuli asterehe kwa amani, Amina,” ameandika Msigwa katika akaunti yake ya Instergram.

Kabla ya kufikwa na umauti, Monica alitembelewa na kaka yake, Rais Magufuli jana tarehe 18 Agosti, 2018.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!