Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Msako wa mashine za EFD waendelea
Habari Mchanganyiko

Msako wa mashine za EFD waendelea

Spread the love

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema itaendelea kufanya ukaguzi wa matumizi za mashine za kutolea risiti za kielektroniki (EFD), ili kuhakikisha kila mfanyabiashara anatoa risiti za EFD na kulipa kodi stahiki. Anaripoti Regina Kelvin …. (endelea).

Hayo yalisemwa jana tarehe 31 Julai, 2018 na Kamishna wa kodi za ndani  Elijah Mwandumbya alipofanya ukaguzi wa kushtukiza katika maduka yaliyopo eneo la Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Mwandumbya aliwataka wafanyabiashara kuacha kutoa sababu ya ubovu wa mashine za EFD kwa kuwa mashine hizo sasa zinafanyakazi vizuri.

“TRA  haitakubali mfanyabishara anayeonesha barua kama sababu ya kutokutoa risiti ya EFD, tatizo la mashine lilikwisha, ni wajibu wa wafanyabiashara kutoa risiti,” amesema  Mwandumbya.

Kamishna Mwandumbya amesema wafanyabiashara wote wanaostahili kutoa Risiti za EFD wanapaswa kutoa kwa kila mauzo wanayofanya kwani tatizo la mashine lilishashughulikiwa na limekwisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!