Wednesday , 1 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Ummy: Serikali isiwe kikwazo
Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy: Serikali isiwe kikwazo

Waziri wa Nchi Ofisi a Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Ummy Mwalimu
Spread the love

TAASISI za serikali zinazohusika na masuala ya ukaguzi na udhibiti wa bidhaa, zimetakiwa kutokuwa kikwazo kwa maendeleo ya wajasiriamali na ujenzi wa viwanda hapa nchini. Anaripoti Regina Kelvin…(endelea).

Agizo hilo limetolewa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akihutubia kwenye mkutano wa wadau wa kujadili mchango wa taasisi za serikali katika kuanzisha na kuboresha viwanda vya chakula nchini.

Waziri Ummy amesema Shirika la Viwango nchini (TBS), Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA) na ofisi ya mkemia mkuu wa serikali kusikilizana katika utekelezaji wa majukumu yao ili kuondoa vikwazo kwa wajasiriamali na ujenzi wa viwanda.

“TBS, TFDA na mamlaka nyingine inabidi msikilizane ili kuondoa vikwazo kwa wafanyabiashara na wawekezaji,” amesema.

Naye Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema serikali itanedelea kuondoa changamoto za wajasiriamali na wawekezaji wa viwanda, lakini amewataka wajasiriamali hao kutobweteka katika uzalishajiwa bidhaa zenye ubora.

“Tunajenga vianda kwa ajili ya kutoa ajira, kuanzisha bishaa zenye ubora na viwango vya kukidhi matakwa ya watanzania na soko la nje ya nchi. Tunachopaswa kufanya tutengeneze viwango vya kiuhalisia. Tunawasaidia lakini Msibweteke,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Habari Mchanganyiko

TMA yapongezwa kuimarisha ubora na usahihi wa taarifa za Hali ya Hewa

Spread the love  WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

error: Content is protected !!