Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wakuliwa wanaoishi karibu ya vituo vya Utafiti kufaidika
Habari Mchanganyiko

Wakuliwa wanaoishi karibu ya vituo vya Utafiti kufaidika

Spread the love

WATAFITI wa mbegu waliopo kwenye vituo 16 vya Utafiti wa mazao mbalimbali hapa nchini wameshauriwa kuhakikisha mbegu wanazozalisha kwanza zinatumiwa na wakulima wanaozunguka vituo vyao na baadae wazifikishe kwa wakulima wengine wa mbali. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) Dk. Geofrey Mkamilo amesema hayo jana kwenye uzinduzi wa ofisi ya TARI iliyopo kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere vya maonesho ya wakulima 88 kanda ya mashariki na kwamba matumizi hayo ya mbegu kwa wakulima wa jirani na vituo yatasaidia wakulima wengine kuona umuhimu wa vituo hivyo.

Amesema kuwa watafiti mbalimbali kupitia vituo hivyo wamekuwa wakitengeneza mbegu mbalimbali zikiwemo za mazao ya chakula na biashara lakini wamekuwa wakifikisha elimu hiyo kwa wakulima waliopo mbali na vituo na kuwaacha wakulima wa maeneo yao jambo ambalo wakati mwingine halileti maana.

“Haiwezekani kukawa na kituo cha utafiti katika eneo halafu wakulima wa eneo husika hawanufaiki na wanaendelea kulima kwa kutumia mbegu za zamani bila kutumia teknolojia nzuri zilizopo,” amesema.

Pia Dk. Mkamilo amesema kuwa kuhimiza matumizi ya mbegu bora kwa wakulima waliopo jirani na vituo vya utafiti itasaidia hata wakulima wengine kutoka maeneo ya mbali kuweza kupata elimu na kujifunza kabla ya kuanza kutumia mbegu na teknolojia za utafiti zinazozalishwa na vituo hivyo.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Injinia Matwew Mtigumwe amewataka wakulima kuzitumia mbegu na teknolojia zinazotolewa na watafiti ili kuweza kuinua sekta ya kilimo na kufikia malengo yanayokusudiwaa.

Injinia Mtigumwe amesema kuwa matumizi ya mbegu zilizopitishwa na watafiti yanaweza kuinua uchumi wa jamii kupitia kilimona pia kufikisha nchi katika suala zima la Uchumi wa Viwanda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

error: Content is protected !!