Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu kupasuliwa kwa mara nyingine
Habari za SiasaTangulizi

Lissu kupasuliwa kwa mara nyingine

Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki akiwa na mkewe nchini Ubelgiji akifanya mazoezi
Spread the love

TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), muda huu atafanyiwa upasuaji mwingine katika mguu wake wa kulia, ikiwa ni mara ya 20 tangu alipoanza kutibiwa baada ya kushambuliwa kwa risasi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Lissu amesambaza ujumbe katika mitandao ya kijamii ulioeleza: “Napenda kuwajulisha kwamba ndani ya nusu saa ijayo ninaingia kwenye operesheni nyingine tena.”

Amesema madaktari wamebaini bakteria katika mguu wake wa kulia ambao uliumizwa sana, hivyo wameamua kumfanyia upasuaji ili kuwaondoa.

Operesheni hiyo inayofanyika nchini Ubelgiji ni ya 20 baada ya ile ya 19 ilifanyika mwezi Machi mwaka huu ikiwa ni mwendelezo wa matibabu aliyokuwa akifanyiwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alikopelekwa akitokea Dodoma baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 akiwa nje ya makazi yake mjini Dodoma Septemba 7, mwaka jana.

Lissu amesema baada ya operesheni huo atafanyiwa upasuaji mwingine baadaye wa kuunga mfupa. “Niseme tu naendelea vizuri sana. Ninawashukuru Watanzania kwa kunitibu, kwani wenye jukumu la kufanya hivyo wamekataa lakini Watanzania hawajanitupa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!