WANAMICHEZO nane wa Cameroon hawaonekani katika makazi yao katika michezo ya Jumuiya madola nchini Australia, maafisa wa timu hiyo wamethibitisha. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Afisa wa habari wa timu ya Cameroon, Simon Molombe amesema kutoonekana kwa wanariadha hao wanaamini wametoroka na kwamba wameripotiwa kwa maafisa wa polisi nchini humo.
Amesema wanyanyua vyuma vya uzito watatu na mabondia watano walionekana mara ya mwisho katika muda tofuati Jumatatu na Juamnne.
Cameroon imesema kundi la wanariadha hao wana viza halali za kudumu hadi Mei 15.
Wanamichezo waliotoweka kambini ni pamoja na Olivier Matam Matam, Arcangeline Fouodji Sonkbou na Petit Minkoumba, wanaonyanyua vyuma vya uzito na mabondia Christian Ndzie Tsoye, Simplice Fotsala, Arsene Fokou, Ulrich Yombo na Christelle Ndiang.
Serikali ya Australia imewaonya wanariadha dhidi ya kukaa zaidi ya muda walioruhusiwa.
Shirikisho la michezo hiyo ya Jumuiya ya madola limesema litaikagua hali hiyo, lakini limeongeza kwamba wanariadha wana “haki ya kusafiri kwa uhuru” kwa viza walizo nazo.
Polisi ya Australia imejulishwa kuhusu hali inavyoendelea, kwa mujibu wa Kate Jones, waziri katika jimbo la Queensland.
Leave a comment