Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Wanamichezo Jumuiya ya Madola ‘wazamia’
Michezo

Wanamichezo Jumuiya ya Madola ‘wazamia’

Spread the love

WANAMICHEZO nane wa Cameroon hawaonekani katika makazi yao katika michezo ya Jumuiya madola nchini Australia, maafisa wa timu hiyo wamethibitisha. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Afisa wa habari wa timu ya Cameroon, Simon Molombe amesema kutoonekana kwa wanariadha hao wanaamini wametoroka na kwamba wameripotiwa kwa maafisa wa polisi nchini humo.

Amesema wanyanyua vyuma vya uzito watatu na mabondia watano walionekana mara ya mwisho katika muda tofuati Jumatatu na Juamnne.

Cameroon imesema kundi la wanariadha hao wana viza halali za kudumu hadi Mei 15.

Wanamichezo waliotoweka kambini ni pamoja na Olivier Matam Matam, Arcangeline Fouodji Sonkbou na Petit Minkoumba, wanaonyanyua vyuma vya uzito na mabondia Christian Ndzie Tsoye, Simplice Fotsala, Arsene Fokou, Ulrich Yombo na Christelle Ndiang.

Serikali ya Australia imewaonya wanariadha dhidi ya kukaa zaidi ya muda walioruhusiwa.

Shirikisho la michezo hiyo ya Jumuiya ya madola limesema litaikagua hali hiyo, lakini limeongeza kwamba wanariadha wana “haki ya kusafiri kwa uhuru” kwa viza walizo nazo.

Polisi ya Australia imejulishwa kuhusu hali inavyoendelea, kwa mujibu wa Kate Jones, waziri katika jimbo la Queensland.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!