Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Chadema amvaa waziri wa mifugo
Habari za Siasa

Mbunge Chadema amvaa waziri wa mifugo

Spread the love

MBUNGE wa Tarime Mjini, Ester Matiko (Chadema) amehoji serikali ni kwanini Mnada wa Magena umefungwa licha ya kuwa na miundombinu yote. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Akiuliza swali jana bungeni,Mbunge huyo alidai kuwa mnada huo uliopo halmashauri ya Mji wa Tarime una miundombinu yote licha ya kufungwa na Serikali bila sababu maalumu.

Mbunge huyo alidai mwaka 2016 aliyekuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, alitembelea mnada huo na kuagiza ufunguliwe.

“Je ni kwanini mnada huo haujafungiliwa mpaka sasa ili kutoa fursa za ajira na kuokoa mapato yanayopotea,” amehoji Matiko.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amesema mnada wa Magena ulikuwa kati ya minada 10 ya mipakani.

Amesema mnada huo ulikamilika kujengwa mwaka 1995 na kufunguliwa mwaka 1996 ambapo ulifanya kazi kwa takribani mwaka mmoja ambapo ng’ombe 104,000 waliuzwa na jumla ya Sh. 260 milioni zilikusanywa kama maduhuli ya Serikali.

Naibu Waziri huyo amesema kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwemo wizi wa mifugo na sababu za kiusalama kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Mara mwaka 1997 iliagiza mnada huo ufungwe.

“Kutokana na hali hiyo, uongozi wa Mkoa wa Mara uliiomba Wizara ya Maendeleo ya Mifugo ya wakati huo ifute mnada wa Magena na Kirumi Check Point iteuliwe kuwa mnada wa mpakani kwa kuwa tayari kuwa kizuizi cha Mto Mara,” amesema.

Hata hivyo, Naibu Waziri huyo amesema Wizara ilikubali ombi la uongozi wa mkoa wa Mara na hivyo ikaanza kujenga mnada eneo la Kirumi sehemu ambayo kuna kizuizi asili cha Mto Mara.

Amesema ujenzi huo umekamilika kwa asilimia 80 na unatarajiwa kufunguliwa mwaka huu mara baada ya kukamilika ujenzi wa kituo cha Polisi cha kuweka umeme.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!