Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Wanachuo waaswa kutotegemea kuajiriwa na Serikali
ElimuTangulizi

Wanachuo waaswa kutotegemea kuajiriwa na Serikali

Spread the love

VIJANA wengi wanaomaliza elimu ya juu wanatakiwa kuachana na fikra za kutaka kuajiriwa na serikali na badala yake wafikirie kutumia elimu yao kwa lengo la kubuni miradi mbalimbali ambayo itawawezesha kujiajiri wenyewe. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Mbali na hilo imeelezwa kuwa bila wanafunzi wa vyuo vikuu nchini kupatiwa elimu ya stadi za maisha ni vigumu kufikia mapinduzi ya kiuchumi kwenye jamii inayowazunguka.

Kauli hiyo imetolewa mara baada ya kubainika idadi kubwa ya wanafunzi wa elimu ya juu pindi wanapohitimu masomo wanashindwa kutumia taaluma yao kuanzisha miradi ya kiuchumi badala yake wanasubiri kuajiriwa.

Akizungumza juzi mjini hapa kwenye mafunzo maalum ya stadi za maisha yaliyotolewa kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Mwezeshaji wa mafunzo hayo kutoka Taasisi ya Green Hope, Manjala Makongoro kwa ushirikiano wa kampuni ya simu za mkononi Vodacom, amesema elimu kuhusu stadi za maisha itamwezesha mwanafunzi kujitambua.

Amebainisha kuwa lazima mwanafunzi wa elimu ya juu kujitambua thamani yake kwenye jamii, hivyo anapaswa kuitumia taaluma yake kama njia ya kuondokana na utegemezi wa kiuchumi.

“Mwanafunzi mwenye kujitambua anapaswa kuwa na tabia ya kujitathimi kwa kila jambo analolifanya kama lina maslahi kwake na kwenye jamii.

“Pia lazima awe mwenye uthubutu wa kufanya maamuzi ya kuachana na jambo ambalo anaona halina maslahi kwake na kutafuta njia bora za kumwezesha kufikia malengo aliyoyakusudia,” ameeleza.

Mwezeshaji huyo amesema taasisi hiyo kwa kushirikiana na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom, imeamua kutoa mafunzo hayo ili kuunga mkono juhudi za serikali katika kuwajengea uelewa vijana waweze kutumia fursa zilizopo kuleta mapinduzi ya kiuchumi.

“Serikali imekuwa ikisisitiza mapinduzi ya viwanda lakini kama wanafunzi wa vyuo vikuu wakikosa ufahamu kwenye stadi za maisha zitakazowawezesha kujiajili, kundi hilo litaachwa nyuma, ” amesema.

Naye Meneja wa Vodacom mkoani Dodoma, Balikulile Mchome, amesema mafunzo hayo yameonyesha kufanikiwa kwani wanafunzi wamekuwa na shauku ya kutaka kufahamu masuala mbalimbali yatayowawezesha kujitegemea kiuchumi baada ya kuhitimu masomo.

“Vijana wameonyesha kuwa na shauku ya kuwa wajasiliamali. Kwetu sisi ni mafanikio kwani kile tulichokilenga kimeonyesha mafanikio,” amesisitiza.

Naye Mooren Minja, ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza anayesomea shahada ya elimu chuoni hapo, amesema mafunzo hayo yamewawezesha kujijengea uwezo wa kujitathimi na kubaini namna ya kukabiliana na changamoto za kiuchumi.

Amesema elimu ya stadi za maisha ni muhimu kwa wanafunzi kwani itamjengea wigo wa kuchanganua mambo yatakayowezesha kufikia lengo alilolikusudia hususan kufikia hatua fulani ya maendeleo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!