Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bavicha wajitosa kulinda hatma ya Chadema
Habari za SiasaTangulizi

Bavicha wajitosa kulinda hatma ya Chadema

Patrick Ole Sosopi, Mwenyekiti wa Bavicha
Spread the love

BARAZA la Vijana la  Chadema (Bavicha) limejiapiza kukulinda chama chao kwa gharama yeyote kwa kile walichodai ni hujuma za kutaka kukifuta na kufungwa kwa viongozi wa chama hicho. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mwenyekiti wa Bavicha, Patrick Ole Sosopi amesema kuwa vijana wa Chadema ndiyo walinzi wa chama hicho ambapo ameahidi kupitia vijana hao chama kitalindwa dhidi ya hujuma.

Amesema kuwa chama hicho kipo kwenye hujuma zilizopangwa makusudi ili chama tawala ambacho ndicho chama dola ambacho kimetani kibaki chama kimoja.

Ole Sosopi amesema kuwa kushikiliwa kwa viongozi wa juu wa chama hicho ni sehemu ya mkakati huo ambapo ameeleza jinsi viongozi hao walivyokamatwa na kufikishwa mahakamani kimya kimya ikiwa muda umeenda hadi kukosa dhamani kuwa ni mkakati wa kuwafunga.

Amesema kuwa hujuma hizo zimemuibua msajili wa vyama vya siasa ambaye amekuwa akitumia mwamvuli huo kutaka kukihujuma chama kwa kutishia kukifuta.

Amemtaja Cyprian Musiba ambaye amekuwa akiwatukana na kukashifu viongozi wa chama hicho bila kuchukuliwa hatua yoyote kisheria ilhali anavunja sheria ambapo anaonekana kuwa sehemu ya mkakati huo.

Mwenyekiti huyo amesema kuwa hawatarudi nyuma kwenye uamuzi watakao uwelekeza kwa wafuasi vijana wa chama hicho.

“Bavicha iliyopo chini yangu sio ile ya Katambi (Patrobas) lakini hata kipindi kile mimi ndiye niliyekuwa nikihamasisha hatua kadhaa kwenye chama. Bavicha hii haitarudi nyuma,” amesema Ole Sosopi.

Wakati huohuo, Ole Sosopi amesema viongozi na wafuasi wa chama hicho wataenda mahabusu kuwafariji na kusherehekea pamoja Sikukuu ya Pasaka kwenye gereza la Segerea jijini Dar es Salaam na gereza la Ruanda Mbeya alikofungwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!