Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga sasa kuja kidigitali
Michezo

Yanga sasa kuja kidigitali

Msemaji wa Yanga, Dismas Ten (kulia) akiwa na Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Charles Mkwasa
Spread the love

KLABU Yanga imezindua kipindi cha televisheni kilichopewa jina la ‘Yanga TV Show’ sambamba na mfumo wa kuwapa habari wanachama wake utakaoitwa ‘Yanga Kidigitali’ vinavyotarajiwa kuanza Aprili Mosi Mwaka huu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kipindi cha Yanga TV Show kitakuwa kinarushwa kupitia kituo cha televisheni cha Azam TV wakati mfumo wa kutoa habari kwa wanachama wa Yanga Kidigitali utakuwa unapitia kampuni ya simu za mkononi za Tigo pamoja ya Prime.

Meneja wa michezo wa Azam Tv, Baruhan Muhuza amesema wameingia makubaliano na klabu ya Yanga ya uanzishwaji wa kipindi hicho baada ya majadiliano ya muda mrefu ili kufanya kipindi hicho kuwa cha tofauti.

“Yanga TV Show itakuja na muonekana mpya na wakipekee kwa kuwa itahusisha wachezaji wa zamani wa klabu hii kufanya uchambuzi katika michezo iliopita na itakayokuja katika Ligi Kuu pamoja na kuwajua mwenendo mzima wa timu inapokuwa ndani na nje ya Uwanja,” amesema Muhuza.

Aidha aliongezea ya kuwa Yanga kuwa na kipindi cha televisheni itakuwa fulsa kwa klabu katika kujiongezea mapato kwa kuwa kipindi kinaweza kupata wadhamini kutokana na kuwa cha tofauti na kufanya klabu hiyo iweze kujiendesha yenyewe kwa kuwa na vyanzo vingi vya mapato.

Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa amesema kuanzisha Yanga TV Show na Yanga Kidigitali ni mikakati ya kuwapa fulsa wanachama wa klabu hiyo kupata habari za timu yao ikiwa pamoja na kujipatia kipacho ambacho kitaifanya waweze kujitegemea kwa kipato.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!