Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Viongozi TSNP wahojiwa saa saba kuhusu Nondo
Habari za SiasaTangulizi

Viongozi TSNP wahojiwa saa saba kuhusu Nondo

Alphonce Lusako, ofisa wa ukaguzi wa haki za binaadamu kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC). Picha ndogo Hellen Sisya, Ofisa Habari wa TSNP
Spread the love

JESHI la Polisi nchi limewahoji viongozi wa Mtandao wa wafunzi (TSNP) kama mashahidi kwenye kesi anayotarajiwa kufunguliwa Mwenyekiti wa mtandao huo Abdul Nondo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Nondo aliripotiwa kutekwa usiku wa Kuamkia Machi 8 Mwaka huu. Jeshi hilo linamtuhumu mwenyekiti huyo kufanya kosa la udanganyifu na kuzua taharuki kwa umma pamoja na wanafunzi wenzake.

Jeshi hilo limewahoji watu wanne ambao ni Alphonce Lusako, ofisa wa ukaguzi wa haki za binaadamu kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), na viongozi wa TSNP akiwemo Hellen Sisya, Ofisa Habari, Paul Kisabo Mkurugenzi wa Idara ya sheria na Malekela Brigthon, ambaye ni Katibu wa Mtandao huo.

Viongozi hao waliowasili kwenye Ofisi za Mkuu wa Makosa Jinai (DCI) majira ya saa 3 asubuhi na kumaliza kuhojiwa saa kumi jioni.

Wakili wa viongozi hao Reginald Martine amesema kuwa wamehojiwa kama sehemu ya ushahidi wa jamhuri na amesema kuwa hakujua kilichoendelea kwenye mahojiana hayo kwa kile kilichodaiwa kuwa shauri hilo lipo kwenye uchunguzi na kwamba anaweza kuvuruga ushahidi.

Ofisa habari wa mtandao huo, Hellen Sisya amesema “Ingawa tunaambiwa uchunguzi unaendelea lakini viongozi waandamizi wa serikali akiwemo Waziri wa mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam walishamhukumu mtuhumiwa hata kabla ya uchunguzi wa mashtaka hayo kumalizika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!