Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Ninje wa Chalenji, apewa Ngorongoro Heroes
Michezo

Ninje wa Chalenji, apewa Ngorongoro Heroes

Ammy Ninje, Kocha wa muda wa Ngorongoro Heroes
Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemteuwa Ammy Ninje kuwa Kocha Mkuu wa muda wa timu ya Taifa ya Vijana chini ya Umri wa Miaka 20, ‘Ngorongoro Heroes’ ambayo inatarajia kucheza michezo miwili ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya dhidi ya Morocco na Msumbiji. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Ninje ambaye hapo awali alikuwa kocha wa muda wa Timu ta Taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’ iliyoshiriki michuano ya Kombe la Chalenji iliyofanyika nchini Kenya katika mwaka uliopita na kuondoshwa katika hatua ya makundi.

Ngorongoro Heroes itacheza na timu ya Taifa ya Vijana ya Morocco Jumamosi ya Machi 17, 2018 na dhidi ya timu ya  Msumbiji Jumatano Machi 21, 2018 michezo yote ikichezwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Kocha huyo ataiongoza Ngorongoro Heroes katika michezo hiyo miwili ya kirafiki kabla ya kuivaa DR Congo katika mchezo wa kuwania kufuzu kombe la Mataifa Afrika kwa vijana chini ya miaka 20 (AFCON U20).

Mchezo huo ambao utachezwa Machi 31 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, na mechi ya marudiano itafanyika baada ya wiki mbili mbili jijini Kinshansha, nchini Congo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!