Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Marekani yachunguza serikali ya JPM
Habari za SiasaTangulizi

Marekani yachunguza serikali ya JPM

Maalim Seif Sharrif Hamad, Katibu Mkuu wa CUF (kulia) akizungumza na wajumbe wa kutoka Marekani katika Makao Makuu ya chama hicho, Zanzibar
Spread the love

WAJUMBE wawili kutoka nchini Marekani kutoka katika kitengo cha Mshauri wa Marekani kinachohusu Siasa na Uchumi wametua nchini kwa kile kinachodhaniwa kuchunguza Serikali ya Tanzania Bara inayoongozwa na Rais John Magufuli na ile ya Mapinduzi Zanzibar chini ya Dk. Ali Mohammed Shein. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Wajumbe hao watajikita katika masuala makuu mawili; hali ya kisiasa pamoja na uchumi. Tayari wajumbe hao wamekutana na Maalim Seif Shariff Hamad, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF).

Taarifa za awali zinaeleza, msukumo huyo unatokana na kuyumba kwa hali ya kisiasa nchini pamoja malalamiko ya kusinyaa kwa uchumi.

Hofu na wasiwasi nchini imeanza kumeya hasa baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ambapo mpaka sasa, watu wamekuwa wakitoweka/kupotea, kukutwa wameuawa pamoja na wengine kujeruhiwa.

Hali hiyo imetia msukumo wa wasiwasi na hata wengine kuhama nchi wakihofia kuuawa. Tayari watu kadhaa wamepata hifadhi ya ukimbizi nje ya Tanzania kutokana na hofu ya kuuawa akiwemo aliyekuwa mwandishi wa gazeti la MwanaHALISI, Ansbert ngurumo ambaye amehifadhiwa nchini Finland.

Miongoni mwa waliopotea na wanaotafutwa na ndugu zao mpaka sasa ni pamoja na Ben Saanane, aliyekuwa msaidizi wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, mwandishi wa Gazeti la Mwananchi, Azory Gwanda.

Kwenye orodha ya watu waliouawa katika mazingira tatanishi ni pamoja na John Daniel, aliyekuwa Katibu wa Chadema Kata ya Hananasifu, Kinondoni Dar es Salaam.

Mwingine ni Alphonce Mawazo aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Geita, Godfrey Lwema aliyekuwa Diwani wa Chadema, Kata ya Namawala Kilombero, Morogoro.

Pamoja na hivyo, baada ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 kumekuwepo na matukio ya wananchi kuuawa na kufungwa kwenye viroba na kasha kutupwa mtoni pamoja na baharini ambapo Jeshi la Polisi likiendelee kukalia ripoti ya mauaji hayo.

Matukio mengine yaliyosisimua Tanzania na dunia ni kushambuliwa kwa risasi 38 Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzania Bungeni ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) Septemba 7, 2017 Dodoma.

Wajumbe hao kutoka Bunge la Marekani ni John Espinoza na Lauren Ladenson wamekutana na Maalim Seif katika Makao Makuu ya CUF yaliyopo Mtendeni, Zanzibar.

Katika ujumbe waki wa Twitter Maalim Seif amesema, Maalim Seif ameeleza kuwa lengo kuu la wajumbe hao ni kuangalia kwa undani hali ya kisiasa Tanzania Bara, Zanzibar na hali ya uchumi kwa jumla.

Anderson Ndambo ambaye ni Ofisa Habari wa CUF akizungumza na MwanaHALISI Online hakuweka wazi siku ama tarehe ya wageni hao kutua nchini, hata hivyo amesema kuwa, mazungumzo kati ya Maalim Seif na wajumbe hao yataelezwa baadaye.

“Kwa kifupi ugeni huu umekuja kwa ajili ya kujadili hali ya kisiasa na uchumi nchini lakini zaidi tutaelezana baadaye,” amesema Ndambo.

Hata hivyo, MwanaHALISI Online limewasiliana na Msemaji wa Serikali Dk. Hassan Abbas ili kujua uwepo pia ratiba ya wajumbe hao.

“…Nyie MwanaHALISI Online nani amewaruhusu mfanye kazi…, mtaumia. Msishindane na serikali. Kwanza nitumie jina lako kwenye meseji,” amesema Dk. Abas

Kumekuwepo na malalamiko ya vyama vya upinzani nchini kuminywa haki ya kufanya siasa lakini pia baadhi ya wananchi wamekuwa wakilalamikia hali mbaya ya uchumi.

Hata hivyo, serikali imekuwa ikitoa takwimu kuonesha uchumi ukiendelea kuimarika siku hadi siku.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!