Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Viongozi TSNP wahojiwa saa saba kuhusu Nondo
Habari za SiasaTangulizi

Viongozi TSNP wahojiwa saa saba kuhusu Nondo

Alphonce Lusako, ofisa wa ukaguzi wa haki za binaadamu kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC). Picha ndogo Hellen Sisya, Ofisa Habari wa TSNP
Spread the love

JESHI la Polisi nchi limewahoji viongozi wa Mtandao wa wafunzi (TSNP) kama mashahidi kwenye kesi anayotarajiwa kufunguliwa Mwenyekiti wa mtandao huo Abdul Nondo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Nondo aliripotiwa kutekwa usiku wa Kuamkia Machi 8 Mwaka huu. Jeshi hilo linamtuhumu mwenyekiti huyo kufanya kosa la udanganyifu na kuzua taharuki kwa umma pamoja na wanafunzi wenzake.

Jeshi hilo limewahoji watu wanne ambao ni Alphonce Lusako, ofisa wa ukaguzi wa haki za binaadamu kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), na viongozi wa TSNP akiwemo Hellen Sisya, Ofisa Habari, Paul Kisabo Mkurugenzi wa Idara ya sheria na Malekela Brigthon, ambaye ni Katibu wa Mtandao huo.

Viongozi hao waliowasili kwenye Ofisi za Mkuu wa Makosa Jinai (DCI) majira ya saa 3 asubuhi na kumaliza kuhojiwa saa kumi jioni.

Wakili wa viongozi hao Reginald Martine amesema kuwa wamehojiwa kama sehemu ya ushahidi wa jamhuri na amesema kuwa hakujua kilichoendelea kwenye mahojiana hayo kwa kile kilichodaiwa kuwa shauri hilo lipo kwenye uchunguzi na kwamba anaweza kuvuruga ushahidi.

Ofisa habari wa mtandao huo, Hellen Sisya amesema “Ingawa tunaambiwa uchunguzi unaendelea lakini viongozi waandamizi wa serikali akiwemo Waziri wa mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam walishamhukumu mtuhumiwa hata kabla ya uchunguzi wa mashtaka hayo kumalizika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

error: Content is protected !!