JESHI la Polisi nchi limewahoji viongozi wa Mtandao wa wafunzi (TSNP) kama mashahidi kwenye kesi anayotarajiwa kufunguliwa Mwenyekiti wa mtandao huo Abdul Nondo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Nondo aliripotiwa kutekwa usiku wa Kuamkia Machi 8 Mwaka huu. Jeshi hilo linamtuhumu mwenyekiti huyo kufanya kosa la udanganyifu na kuzua taharuki kwa umma pamoja na wanafunzi wenzake.
Jeshi hilo limewahoji watu wanne ambao ni Alphonce Lusako, ofisa wa ukaguzi wa haki za binaadamu kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), na viongozi wa TSNP akiwemo Hellen Sisya, Ofisa Habari, Paul Kisabo Mkurugenzi wa Idara ya sheria na Malekela Brigthon, ambaye ni Katibu wa Mtandao huo.
Viongozi hao waliowasili kwenye Ofisi za Mkuu wa Makosa Jinai (DCI) majira ya saa 3 asubuhi na kumaliza kuhojiwa saa kumi jioni.
Wakili wa viongozi hao Reginald Martine amesema kuwa wamehojiwa kama sehemu ya ushahidi wa jamhuri na amesema kuwa hakujua kilichoendelea kwenye mahojiana hayo kwa kile kilichodaiwa kuwa shauri hilo lipo kwenye uchunguzi na kwamba anaweza kuvuruga ushahidi.
Ofisa habari wa mtandao huo, Hellen Sisya amesema “Ingawa tunaambiwa uchunguzi unaendelea lakini viongozi waandamizi wa serikali akiwemo Waziri wa mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam walishamhukumu mtuhumiwa hata kabla ya uchunguzi wa mashtaka hayo kumalizika.
Leave a comment