Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Utafiti wa wafanyakazi wa ndani wapigwa ‘stop’
Habari Mchanganyiko

Utafiti wa wafanyakazi wa ndani wapigwa ‘stop’

Prof. Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu
Spread the love

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Tekinolojia, imeipiga marufuku Taasisi ya Haki za Binadamu kufanya utafiti wa unyanyasaji watumishi wa ndani wa kitanzania wanaofanya kazi nchini Omani na Umoja wa Falme za Kiarabu, anaandika Angel Willium.

Ofisa wa Wizara ya Elimu Sayansi na Tekinolojia, William Kindeketa ambaye ni mwanasayansi amesema watafiti hao hawakufata utaratibu na utafiti umefanyika hapa nchini waliwahoji wafanyakazi walioenda katika nchi hizo.

“Katika nchi yoyote kukitaka kufanya tafiti ni lazima ufate taratibu zinazotakiwa kufuatwa ikiwemo kujaza fomu ya maombi na kupitiwa na watalaamu ili kujua kama imekidhi vigezo,” amesema Kindeketa.

Kwa upande wa Taasisi ya Haki za Binadamu, kupitia kwa Ofisa wake Audrey Kawire amesema leo walitaka kuzindua ripoti ya “kufanya kazi mithili ya roboti,” unyanyasaji wa watumishi wa ndani wa kitanzania nchini Oman na Umoja wa Falme za Kiarabu, lakini Maofisa wa Costech wamesema tusizindue kwa sababu atukufata utaratibu wakufanya utafiti.

Pia Kawire amesema waliruhusiwa na Wizara ya Mambo ya Nje kutoa ripoti hiyo, hivyo walifuata taratibu zote zinazotakiwa katika utafiti, watu wa Costech wamekuja leo asubuhi walivyotaka kuzindua, wakafanya nao mazungumzo na yalikuwa mazuri, tafiti hii wamefanya wenyewe na wakaandika barua kwa serikali.

Taasisi ya Haki za Binadamu ni ya kimataifa, inayojitegemea ambayo inafanya kazi kama sehemu ya harakati zenye nguvu za kusimamia utu na heshima ya binadamu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!