Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Walemavu wapaza sauti zao
Habari Mchanganyiko

Walemavu wapaza sauti zao

Jenister Mhagama, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu
Spread the love

CHAMA cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) kinatarajia kuanzisha mradi maalum utakaosaidia viziwi na watendaji wa serikali za mitaa kufanya ufuatiliaji wa matumizi ya mafungu ya fedha za walemavu kwa kutoa mafunzo katika mikoa mitatu Mwanza, Arusha na Morogoro, anaandika Jovina Patrick.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Msafiri Mhando, Mratibu wa Miradi CHAVITA, amesema kumekuwepo na mafanikio katika malengo yao ikiwamo kuimarisha taasisi hiyo kwa kuboresha sera, kanuni na kurekebisha katiba.

Amesema bado kuna changamoto nyingi zinazokwamisha walemavu hao ikiwamo serikali na jamii kwa ujumla kutotilia mkazo utumiaji wa lugha za alama katika utoaji wa elimu pamoja na taarifa ya habari.

Kwa hiyo amesema CHAVITA kwa kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society (FCS) itaanza kuendesha mkakati wa kutoa mafunzo kwa watendaji wa serikali za mitaa katika mikoa hiyo mitatu ili kupunguza changamoto hizi kwa walemavu hao.

Mradi huu utatekelezwa kwa muda wa miezi sita na CHAVITA imetenga 80,000,000/= kwa ajili ya kuutekeleza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari Mchanganyiko

Shahidi aeleza namna Nathwani alivyomjeruhi jirani yake

Spread the loveMSIMAMIZI wa Msikiti wa Wahindi Lohana aitwae, Ankit Dawda (32)...

error: Content is protected !!