Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Walemavu wapaza sauti zao
Habari Mchanganyiko

Walemavu wapaza sauti zao

Jenister Mhagama, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu
Spread the love

CHAMA cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) kinatarajia kuanzisha mradi maalum utakaosaidia viziwi na watendaji wa serikali za mitaa kufanya ufuatiliaji wa matumizi ya mafungu ya fedha za walemavu kwa kutoa mafunzo katika mikoa mitatu Mwanza, Arusha na Morogoro, anaandika Jovina Patrick.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Msafiri Mhando, Mratibu wa Miradi CHAVITA, amesema kumekuwepo na mafanikio katika malengo yao ikiwamo kuimarisha taasisi hiyo kwa kuboresha sera, kanuni na kurekebisha katiba.

Amesema bado kuna changamoto nyingi zinazokwamisha walemavu hao ikiwamo serikali na jamii kwa ujumla kutotilia mkazo utumiaji wa lugha za alama katika utoaji wa elimu pamoja na taarifa ya habari.

Kwa hiyo amesema CHAVITA kwa kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society (FCS) itaanza kuendesha mkakati wa kutoa mafunzo kwa watendaji wa serikali za mitaa katika mikoa hiyo mitatu ili kupunguza changamoto hizi kwa walemavu hao.

Mradi huu utatekelezwa kwa muda wa miezi sita na CHAVITA imetenga 80,000,000/= kwa ajili ya kuutekeleza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!