Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Walemavu wapaza sauti zao
Habari Mchanganyiko

Walemavu wapaza sauti zao

Jenister Mhagama, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu
Spread the love

CHAMA cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) kinatarajia kuanzisha mradi maalum utakaosaidia viziwi na watendaji wa serikali za mitaa kufanya ufuatiliaji wa matumizi ya mafungu ya fedha za walemavu kwa kutoa mafunzo katika mikoa mitatu Mwanza, Arusha na Morogoro, anaandika Jovina Patrick.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Msafiri Mhando, Mratibu wa Miradi CHAVITA, amesema kumekuwepo na mafanikio katika malengo yao ikiwamo kuimarisha taasisi hiyo kwa kuboresha sera, kanuni na kurekebisha katiba.

Amesema bado kuna changamoto nyingi zinazokwamisha walemavu hao ikiwamo serikali na jamii kwa ujumla kutotilia mkazo utumiaji wa lugha za alama katika utoaji wa elimu pamoja na taarifa ya habari.

Kwa hiyo amesema CHAVITA kwa kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society (FCS) itaanza kuendesha mkakati wa kutoa mafunzo kwa watendaji wa serikali za mitaa katika mikoa hiyo mitatu ili kupunguza changamoto hizi kwa walemavu hao.

Mradi huu utatekelezwa kwa muda wa miezi sita na CHAVITA imetenga 80,000,000/= kwa ajili ya kuutekeleza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!