Saturday , 4 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwenyekiti bodi ya maziwa ageuka ‘bubu’
Habari Mchanganyiko

Mwenyekiti bodi ya maziwa ageuka ‘bubu’

William Ole Nasha, Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi
Spread the love

WAJUMBE wa Baraza la Wadau wa Maziwa Tanzania wamelalamikia bodi ya maziwa kuendeshwa bila wajumbe wake kwa miaka miaka mitatu sasa, anaandika Dany Tibason.

Wametoa malalamiko hayo leo muda mfupi baada ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha, kufungua mkutano wa 13 wa baraza hilo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Veta mjini Dodoma.

Dk. Aichi Kitilyi ambaye ni mwenyekiti wa bodi ameuambia mkutano huo kuwa hawezi kujibu baadhi ya hoja kwa kuwa hakuna viongozi wa bodi.

Amesema bodi yake haina viongozi na kwamba hataweza kujibu jambo lolote katika mkutano huo.
Dk. Kitilyi amesema muda mrefu bodi hiyo haina viongozi na kwamba na kwamba wameishatuma maombi kwa waziri husika.

“Kutokana na kuwa mpaka sasa bodi ya maziwa haina viongozi mimi hapa siwezi kujibu jambo lolote ambalo lilitokana na mkutano wa baraza la wadau wa maziwa ila ninaweza kutoa ushauri kama mdau wa kawaida na hii ni kwa mujibu wa sheria inayounda bodi ya maziwa” amesema Dk. Aichi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

error: Content is protected !!