Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Masogange ana kesi ya kujibu Kisutu
Habari Mchanganyiko

Masogange ana kesi ya kujibu Kisutu

Agnes Masogange akiwasili mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema msanii wa filamu nchini, Aggnes Masogange ana kesi ya kujibu kwenye mashtaka yake ya matumizi ya dawa za kulevya, anaandika Faki Sosi.

Leo Hakimu Mkazi Wilbard Mashauri ametoa uamuzi huo baada ya upande wa Jamhuri kumaliza kuwasilisha ushahidi wake mahakamani hapo.

Ushahidi huo ulitolewa na askari wa Jeshi la Polisi, Sospiter kutoka ofisi ya upelelezi ya kituo kikuu cha Polisi kanda Maalumu ya Dar es Salaam.

Sospiter alidai mahakamani hapo kuwa baada ya kumpekuwa mtuhumiwa Masogonge alimkabidhi askari wa kike (WP), Judicy na kwenda naye kwa mkemia kwa ajili ya kupimwa mkojo.

Hakimu Mashauri alimuuliza mtuhumiwa baada ya kumkuta na hatia kwamba ni kwa namna gani atajitetea mahakamani hapo kati ya njia tatu ya kuwasilisha kiapo, kuleta mashahidi au kukaa kimya.

Mtuhumiwa Masogange aliomba kuleta kiapo na kuleta mashahidi watatu mahakamani hapo.
Kesi hiyo itatajwa tena Oktoba 12 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!