Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Sh. bilioni 1.5 zanufaisha wakulima
Habari Mchanganyiko

Sh. bilioni 1.5 zanufaisha wakulima

Matrekta ya kilimo
Spread the love

TAASISI ya kifedha ya inayohusika na kukopesha mashine mbalimbali ikiwemo matrekta (EFTA), imeahidi kuendelea kuboresha huduma hizo ili kuongeza nguvu za kukuza uchumi wa viwanda nchini, anandika Christina Haule.

Meneja wa taasisi ya EFTA, Martin Jeremia amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa ambapo amesema tangu wameanza kutoa huduma mwaka 2016 hadi sasa wameshatoa mikopo yenye thamani ya Sh. bilioni 1.5 kwa wakopaji 30.

Jeremia amesema kuwa hadi sasa wametoa mikopo kwa wakopaji mbalimbali wa mashine tofauti ikiwemo matrekta kwa wakulima hao 30 kutoka mkoa wa Morogoro na Dodoma (Kibaigwa), kwa kuwa wana masharti nafuu na riba ndogo ya mkopo ukilinganisha na watu wengine.

Aidha, amesema mashine zinazokopeshwa zinaanzia kiasi cha Sh. mil 20 hadi 220 na kwamba wanakopesha sekta ya elimu, afya, kilimo na biashara kwa vifaa vya ujasiriamali na kuwataka kulipa riba ya 17% na marejesho ya mkopo katika kipindi cha miaka mitatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

Habari Mchanganyiko

Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Greyhorse zasaini mkataba wa bil.7.4

Spread the loveTAASISI ya Mwalimu Nyerere (MNF) imesaini mkataba wa miaka 10...

error: Content is protected !!