Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tundu Lissu: Hatutanyamaza
Habari za SiasaTangulizi

Tundu Lissu: Hatutanyamaza

Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)
Spread the love

MARA baada ya kuachiwa huru na mahakama, Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, ametupa dongo lingine kwa Rais John Magufuli kwa kumwambia kuwa watanyamaza wakiwa wafu, anaandika Hellen Sisya.

Lissu alipoachiwa na mahakama alienda moja kwa moja Makao Mkuu ya Chadema, ambako alikutana waandishi wa habari, katika mkutano huo pamoja na mambo mengine amesema: “Mwambieni Magufuli (Rais John Magufuli), tutanyamaza tukiwa wafu.”

Akiongea kwa kujiamini Lissu amesema, “wanataka tunyamaze ili waendeshe nchi hii wanavyotaka wao, Taifa hili ni la mfumo wa vyama vingi, tunayo haki ya kufanya mikutano, tunayo haki ya kufanya maandamano na tunayo haki ya kutoa maoni yetu. Kwa msingi huo hakuna wa kutunyamazisha, nchi hii siyo mali ya mtu binafsi.”

Amesema, “naomba niweke wazi kabisa. Hakuna gereza, wala mahabusu, wala polisi, wala usalama wa taifa, wala Magufuli na wala mtu yeyote atakayetunyamazisha. Narudia. “Hatutakubali kunyamazishwa. Kwa sababu, tukinyamaza kwa kuogopa mahabusu, tukaogopa magereza, tukaogopa mabomu ya mapolisi, tukanyamaza. Nchi hii, inaangamia.”

Kwa mujibu wa Lissu, hicho ndicho wanachotaka. Alisema, “wanataka tunyamaze ili waendeshe nchi wanavyotaka wao.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!