Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bavicha wamnanga Rais Magufuli
Habari za Siasa

Bavicha wamnanga Rais Magufuli

Spread the love

BARAZA la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha) limemtaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli apunguze kutoa kauli zinazojenga chuki mioyoni mwa wa Tanzania, anaandika Jovina Patrick.

Akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya Chadema,  Julius Mwita ambaye ni katibu mkuu wa Bavicha amsema kauli mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa na Rais Magufuli ni hatari kwa umoja wa kitaifa.

“Rais Magufuli anapofurahia kupongezwa kwa mazuri pia akubali kukosolewa, kushauriwa na kupokea maoni, mawazo mbadala,” amesema.

Mwita amedai kuwa wananchi wanajenga chuki kutokana na kauli za Raisi na maelekezo yake, miongoni mwa kauli hizo ikiwemo kauli aliyoitoa kuhusu kuzuia mikutano ya hadhara ya vyanma vya siasa, huku wabunge na viongozi wa CCM wakitumia jukwaa la urais kufanyia mikutano yao.

“Je, CCM imekufa kiasi ambacho haiwezi kufanya mikutano yake yenyewe bila kutegemea mbeleko ya jukwaa la Urais?” Amehoji Mwita.

Aidha, Mwita ameshangazwa na kitendo cha Rais Magufuli kusema “wanasiasa wachunge midomo yao” wakati akijibu ushauri wa waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa, kuhusu kupelekwa mahakamni na kushtakiwa kwa masheikh wanaoshikiliwa mahabusu kwa muda mrefu sasa.

Amesema kuna ombwe kubwa la kiuongozi serikalini ambalo linasababisha wateule wa rais kulewa madaraka na kushiriki uvunjifu wa sheria kwa lengo la kumridhisha rais.

“Tunaunga mkono kauli iliyotolewa na Halima Mdee, mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema kuhusu wasichana wanaopata ujauzito kupewa fursa ya elimu baada ya kujifungua.

“Tunamwambia Rais Magufuli kuwa nchi inaendelea kuvimba na hatua za kuzuia kuvimba huku zisipochukuliwa, ni wazi hatutakuwa salama kabisa katika taifa hili,” amesisitiza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!