Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Silinde awavaa matrafiki ‘wezi’
Habari Mchanganyiko

Silinde awavaa matrafiki ‘wezi’

Askari wa usalama barabarani akiwa kazini
Spread the love

MSEMAJI wa Kambi Rasimi ya Upinzani Bungeni, wa masuala ya fedha na uchumi David Silinde, ameitaka serikali kuchukua hatua dhidi ya askari wa usalama barabarani ambao hufanya kazi bila weledi na kuwabambikizia makosa watu kwa lengo la kuomba rushwa, anaandika Dany Tibason.

Silinde ameyasema hayo wakati akiwasilisha Muswada wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2017/2018, ambapo amedai kuwa ana taarifa kuwepo kwa utaratibu usio rasmi wa kuwapangia maofisa usalama barabarani kukamata magari na kukusanya kiwango maalum cha faini.

“Askari wa usalama barabarani wamekuwa wakisema kuwa wanalazimishwa kupeleka kiasi cha fedha kitokanacho na makusanyo ya faini za makosa ya barabarani, wasipofanya hivyo askari hao hunyimwa mafunzo au kuondolewa katika kitengo cha usalama barabarani,” amesema.

Katika hatua nyingine hatua nyingine, Silinde amekosoa uamuzi wa serikali wa kurasimisha wafanyabaiashara ndogo ndogo (machinga). wakiwemo Mama lishe na washehereshaji (MC) ambapo alidai uamuzi huo unalenga kuwabebesha mzigo wa kodi wajasiriamali hao wenye mitaji midogo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Balile aukwaa uenyekiti wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

Habari Mchanganyiko

Jeshi la Uhifadhi kujengewa uwezo zaidi

Spread the love  WIZARA ya Maliasili na Utalii imejipanga vyema kuendelea kulijengea...

Habari Mchanganyiko

Wanavyuo Dodoma waonja utamu wa chimbo la nyuki

Spread the love  TAMASHA la Chimbo la Nyuki lililofanyika katika Ukumbi wa...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

error: Content is protected !!