Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Silinde awavaa matrafiki ‘wezi’
Habari Mchanganyiko

Silinde awavaa matrafiki ‘wezi’

Askari wa usalama barabarani akiwa kazini
Spread the love

MSEMAJI wa Kambi Rasimi ya Upinzani Bungeni, wa masuala ya fedha na uchumi David Silinde, ameitaka serikali kuchukua hatua dhidi ya askari wa usalama barabarani ambao hufanya kazi bila weledi na kuwabambikizia makosa watu kwa lengo la kuomba rushwa, anaandika Dany Tibason.

Silinde ameyasema hayo wakati akiwasilisha Muswada wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2017/2018, ambapo amedai kuwa ana taarifa kuwepo kwa utaratibu usio rasmi wa kuwapangia maofisa usalama barabarani kukamata magari na kukusanya kiwango maalum cha faini.

“Askari wa usalama barabarani wamekuwa wakisema kuwa wanalazimishwa kupeleka kiasi cha fedha kitokanacho na makusanyo ya faini za makosa ya barabarani, wasipofanya hivyo askari hao hunyimwa mafunzo au kuondolewa katika kitengo cha usalama barabarani,” amesema.

Katika hatua nyingine hatua nyingine, Silinde amekosoa uamuzi wa serikali wa kurasimisha wafanyabaiashara ndogo ndogo (machinga). wakiwemo Mama lishe na washehereshaji (MC) ambapo alidai uamuzi huo unalenga kuwabebesha mzigo wa kodi wajasiriamali hao wenye mitaji midogo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!