Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli amwambia Makonda “chapa kazi”
Habari za SiasaTangulizi

Magufuli amwambia Makonda “chapa kazi”

John Magufuli, Rais wa Tanzania (kulia) akiwa na Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Spread the love

RAIS John Magufuli amemwambia Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, “endelea kuchapa kazi” na anamtaka aamini kuwa ni yeye rais anayepanga, wala sio kushauriwa na mtu yeyote, anaandika Pendo Omary.

Makonda amekuwa katika kipindi cha kukabiliwa na tuhuma nzito za kumiliki vyeti vinavyotajwa kuwa vimetokana na jina la mtu mwingine aitwae Paul Christian, aliyefaulu mtihani wa taifa wa Kidato cha Nne, Shule ya Sekondari ya Pamba, jijini Mwanza.

Isitoshe, Ijumaa ya wiki iliyopita, alijiongezea mzigo wa kashfa alipofuatana na polisi wenye silaha kiasi cha saa 5 usiku na kuvamia kituo cha habari cha Clouds Media, kilichopo Mikocheni, na kutaka kulazimisha kurushwa kipindi cha SHILAWADU kwa namna atakavyo.

Bila ya shaka, Rais Magufuli kwa kutambua yote hayo, na kwa vile ameamua kuendelea kumkingia kifua mteule wake huyo kwa kuwa hajaamua kumbadilisha, ndani ya tuhuma hizo, leo asubuhi ametoa tamko hilo akisema kuwa “kama kuandikwa kwenye mitandao na magazetini, hata mimi naandikwa, kwa hiyo nijiuzulu?”

“Suala la kuandikwa sio tija kwangu… tunapoteza muda. Sipangiwi cha kufanya, mimi najiamini hata fomu ya kugombea urais nilichukua peke yangu sikushauriwa na mtu,” amesema wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa makutano ya barabara eneo la Ubungo, jijini Dar es Salaam.

Makutano hayo yanakutanisha barabara kuu ya Morogoro kuunganishwa na Mandela inayotokea Bandari ya Dar es Salaam na Sam Nujoma inayoishia Mwenge. Ujenzi huo ni sehemu ya mradi mkubwa unaofadhiliwa kwa njia ya mkopo na Benki ya Dunia (WB).

Ujenzi huo utahusu barabara ya urefu wa kilomita moja kutoka makutano ya Ubungo kwa kila upande wa barabara hizo kuu zinazopitia makutano ya Ubungo. Ni mradi unaogharimu Sh. 188 bilioni; Benki ya Dunia ikichangia Sh. 186.72 bilioni kwa njia ya mkopo, wakati Sh. 1.96 bilioni zikitolewa na serikali ya Tanzania. Mradi utatekelezwa na kampuni ya China ambayo haikutajwa lakini muda wake ni miezi 30.

Rais wa Benki ya Dunia, Dk. Jim Yong, alihudhuria hafla hiyo na baadaye kuwa na mazungumzo ya faragha na Rais Magufuli, Ikulu ya Magogoni.

Katika hafla hiyo pia alikuwepo Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob, aliyechaguliwa Novemba mwaka jana kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema); na Rais Magufuli alimtambua akisema anampongeza kwa ushirikiano unaojali maendeleo ya nchi ambayo ndio wananchi wanayotumaini kutoka kwa viongozi wao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!