Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wiki ya nenda kwa Usalama yafutwa
Habari Mchanganyiko

Wiki ya nenda kwa Usalama yafutwa

Spread the love

SERIKALI kupitia Baraza la taifa la usalama barabarani, limetangaza kuifuta sherehe za wiki ya nenda kwa usalama barabarani, iliyokuwa ikifanyika kila mwaka. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Naibu waziri wa mambo ya Ndani, Hamad Yusuf Masauni, amewaambia waandishi wa habari mjini Dodoma, kuwa hatua hiyo ya serikali inatokana na ukweli kuwa sherehe hizo hazijasaidia kuondoa; na au kupunguza tatizo la ajali nchini.

Naibu waziri huyo anasema, “wiki ya usalama barabarani hutumia mabilioni ya shilingi kila mwaka, lakini pamoja na fedha hizo kutumika, bado ajali zimeendelea kuwapo.”

MwanaHALISI Online limeelezwa kuwa tangu Rais John Pombe Magufuli aingie madarakani, Novemba mwaka 2015, amekuwa na utaratibu wa kufuta sherehe kadhaa kwa kisingizio cha kupunguza gharama.

Katika hali ambayo imewaacha wengi mdomo wazi, ni hatua yake ya hivi karibuni ya kufuta sherehe za uhuru wa Tanganyika, zilizokuwa zimepangwa kufanyika tarehe 9 Desemba.

Taarifa iliyotolewa na waziri mkuu wa Jamhuri, Kasim Majaliwa, baada ya Rais John Pombe Magufuli, kuagiza kufutwa kwa sherehe hizo, kiasi cha Sh. 995.1 milioni zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya sherehe za uhuru, zielekezwe kwanye hospitali mkoani Dodoma. Sherehe nyingine zilizofutwa, ni sherehe za siku ya Ukimwi duniani.

“Hospitali hiyo itakayojengwa katika eneo la kati ya barabara ya kwenda Hombolo na Chamwino kwenye barabara ya kwenda Dar es Salaam, itakuwa inawahudumia wakazi wa mkoa wa Dodoma pamoja na wananchi wengine watakaokuwa mkoani humo,”  ameeleza waziri mkuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!