KAULI ya Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwamba, ni marufuku madaktari, wakunga na wauguzi nchini kufukuzwa ama kusimamishwa ovyo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).
Kabla ya kauli ya Ummy, Mch. Peter Msigwa, alimlalamikia waziri huyo kwamba, Ally Hapi, Mkuu wa Mkoa wa Iringa amekuwa akifanya ziara kuwadhalilisha wataalamu, jambo ambalo limesababisha wataalamu wengi wa afya kukimbia hivyo kuongeza tatizo la huduma ya afya mkoani humo.
Mch. Msigwa alifikisha mashitaka hayo bungeni alipokuwa akichangia hotuba ya wizara hiyo juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/20.
Kutokana na kauli hiyo, Waziri Ummy amesepiga marufuku ya kubughudhi watumishi hao wakati akihitimisha hotuba ya bajeti ya wizara yake tarehe 8 Mei 2019.
Amesema, kama daktari, muuguzi au mkunga amekosea, wapelekwe kwenye mabaraza yao ambayo ndiyo yanashughulikia suala la nidhamu kwa kada hiyo ya wstumishi.
“Kutokana na hali halisi ilivyo, muuguzi mmoja anafanya kazi ambayo ingefanywa na wauguzi watano na madaktari wanafanya kazi hivyo si vema kuwakatisha tamaa.
“Sisi kwa kutambua umuhimu wao tutaendelea kuwatetea wauguzi na madaktari wetu, tusiwakatishe tamaa na isitoshe hao wenye fedha hawaendi kutibiwa kwenye hizo hospitali za Serikali, matokeo yake wanaoumia ni watanzania,” amesema Waziri Ummy.
Leave a comment