Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wapinzani kujitoa uchaguzi serikali za mitaa, kwaitesa CCM
Habari za SiasaTangulizi

Wapinzani kujitoa uchaguzi serikali za mitaa, kwaitesa CCM

Humphrey Polepole, Aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM
Spread the love

HATUA ya vyama nane vya upinzani kujitoa katika kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2019, ilishtua Chama cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 18 Januari 2020 na Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, wakati akizungumza katika darasa la itikadi kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, jijini Dar es Salaam.

Polepole amesema CCM ilipata mshtuko kwa kuwa, haikutegemea kama vyama hivyo vya upinzani vingechukua hatua hiyo.

Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi CCM amesema, chama chake kilijipanga kufanya kampeni kwa ajili ya kuchuana katika uchaguzi huo.

“Walipojitoa tumebaki CCM, tulikuwa tunawasubiri, tumejipanga kupiga kampeni hatari lakini wamejitoa wote. Tumepata mshutuko sababu nilikuwa najua nitapiga hapa, nitapiga kule lakini hakuna,” ameeleza Polepole.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ACT-Wazalendo, Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), ni miongoni mwa vyama nane vilivyosusia uchaguzi huo uliofanyika tarehe 24 Novemba 2019, kwa maelezo kwamba mchakato wake ulikuwa unapendelea wagombea wa CCM.

Katika uchaguzi huo, CCM ilishinda kwa asilimia 99.9 baada ya wagombea wake katika nafasi za uenyekiti wa kijiji, serikali za mitaa na kitongoji kupita bila kupingwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!