Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wapiga debe Dar jino kwa jino na Polisi
Habari Mchanganyiko

Wapiga debe Dar jino kwa jino na Polisi

Lucas Mkondya, Kaimu Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam
Spread the love

JESHI la Polisi Kanda maalum ya jijini Dar es Salaam limeahidi kupambana na wapiga debe katika vituo mbalimbali vya mabasi na kuwakamata, anaandika Irene Emmanuel.

Hayo yamesemwaka leo na Kamanda wa Polisi kanda hiyo, Lucas Mkondya na kewamba kazi ya kuwasaka wapiga debe imeanza katika vituo vya mabasi.

Akizungumza na MwanaHALISI online, Mkondya amesema kuna mbinu nyingi ambazo watazitumia kupambana na wapiga debe hadi kuhakikisha wameondoka wote.

Amesema hawezi kusema mbiunu watakazotumia katika kufanikisha kazi hiyo, lakini akaahidi kwamba haitakuwa na kikomo.

‘Tukiwatoa huku wakajidanganya kukimbilia mtaani watakutana na sisi tena, kwa hiyo wao wafanye kazi zilizo halali na siyo za uhalifu kwani tutapambana nao.,” Mkondya ameeleza.

Amesema tayari wameishaanza kazi katika baadhi ya vituo vya mabasi ikiwemo Mwenge jijini Dar es Salaam.

Hii siyo mara ya kwanza jeshi la polisi kupiga marufuku uwepo wa wapiga debe katika vituo vya mabasi bila mafanikio.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!