Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Waliokutwa na madini kinyume na sheria, wakwepa kifungo
Habari Mchanganyiko

Waliokutwa na madini kinyume na sheria, wakwepa kifungo

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu miaka mitatu jela ama kulipa faini ya Sh. 24 milioni wafanyabiashara wawili wa madini baada ya kukiri kosa la kukutwa na madini ya Coloured Gemstones yenye thamani ya Dola za Kimarekani 1.8 milioni. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Pia mahakama hiyo imeamuru madini hayo yataifishwe. Hata hivyo, washtakiwa hao wameweza kuepuka kutumikia kifungo hicho baada ya kulipa faini hiyo.

Hukumu hiyo, imetolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustino Rwizire baada ya Wakili wa Serikali Mkuu, Joseph Pande kuwasomea mashtaka mawili washtakiwa hao ambapo walikiri makosa yao.

Baada ya kukiri makosa yao, Mahakama iliradhimika kuhamia maeneo ya Msasani Kinondoni Dar es Salaam ambapo vielelezo vya kesi hiyo vilikuwepo, ambapo kesi iliendeshwa na washtakiwa kutiwa hatiani. Washitakiwa hao ni Aazam Nazim (Raia wa India) na Ango Mbossa raia wa Tanzania.

Hakimu Rwizire hivyo alimtaka kila mshtakiwa kulipa faini ya Sh. 6 milioni kwa kila kosa ama kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela katika kila kosa.

Kwa kuwa kila mshtakiwa anakabiliwa na mashtaka mawili hivyo kila mshtakiwa atapaswa kutoa faini ya Sh. 12 milioni iwapo atashindwa atatumikia kifungo cha miaka mitatu jela kwa kuwa vifungo hivyo vinaenda sambamba.

Washtakiwa wanadaiwa kutenda makosa yao kati ya January 2017 na June 2018 katika maeneo ya Misisiri A eneo la Mwananyamala.

Wanadaiwa kukutwa na madini aina ya Coloured Gemstones kilogramu 75,920.04 yenye thamani
ya Dola za Kimarekani 1,795,687.87.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!