Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waliokutwa na madini kinyume na sheria, wakwepa kifungo
Habari Mchanganyiko

Waliokutwa na madini kinyume na sheria, wakwepa kifungo

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu miaka mitatu jela ama kulipa faini ya Sh. 24 milioni wafanyabiashara wawili wa madini baada ya kukiri kosa la kukutwa na madini ya Coloured Gemstones yenye thamani ya Dola za Kimarekani 1.8 milioni. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Pia mahakama hiyo imeamuru madini hayo yataifishwe. Hata hivyo, washtakiwa hao wameweza kuepuka kutumikia kifungo hicho baada ya kulipa faini hiyo.

Hukumu hiyo, imetolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustino Rwizire baada ya Wakili wa Serikali Mkuu, Joseph Pande kuwasomea mashtaka mawili washtakiwa hao ambapo walikiri makosa yao.

Baada ya kukiri makosa yao, Mahakama iliradhimika kuhamia maeneo ya Msasani Kinondoni Dar es Salaam ambapo vielelezo vya kesi hiyo vilikuwepo, ambapo kesi iliendeshwa na washtakiwa kutiwa hatiani. Washitakiwa hao ni Aazam Nazim (Raia wa India) na Ango Mbossa raia wa Tanzania.

Hakimu Rwizire hivyo alimtaka kila mshtakiwa kulipa faini ya Sh. 6 milioni kwa kila kosa ama kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela katika kila kosa.

Kwa kuwa kila mshtakiwa anakabiliwa na mashtaka mawili hivyo kila mshtakiwa atapaswa kutoa faini ya Sh. 12 milioni iwapo atashindwa atatumikia kifungo cha miaka mitatu jela kwa kuwa vifungo hivyo vinaenda sambamba.

Washtakiwa wanadaiwa kutenda makosa yao kati ya January 2017 na June 2018 katika maeneo ya Misisiri A eneo la Mwananyamala.

Wanadaiwa kukutwa na madini aina ya Coloured Gemstones kilogramu 75,920.04 yenye thamani
ya Dola za Kimarekani 1,795,687.87.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!